Swali: Mama yangu amefariki na nataka kumzawadia thawabu zangu. Je, nimuombee du´aa, nimsomee Qur-aan, nimtolee swadaqah au nimsomee al-Faatihah?
Jibu: Mtolee swadaqah. Bwana mmoja alimwambia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mama yangu amekufa. Nadhani kuwa lau angeliweza kutamka basi angetoa swadaqah. Je, nimtolee swadaqah?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Ndio.”[1]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Anapofariki mwanadamu basi matendo yake hukatika isipokuwa mambo matatu; swadaqah yenye kuendelea, elimu ambayo watu wananufaika nayo au mtoto mwema mwenye kumuombea du´aa.”[2]
Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) amepokea kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh kutoka kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba kuna mwanamke alimuuliza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kama anatakiwa kulipa siku za mama yake za Ramadhaan? Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akajibu:
“Unaonaje lau mama yako angelikuwa na deni ungelimlipia nalo? Deni la Allaah lina haki zaidi kulipwa.”[3]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Anayekufa na ameacha swawm anayodaiwa, basi atafungiwa na walii wake.”[4]
Kuhusu kumsomea Qur-aan, kukiwemo al-Faatihah, ni jambo halikuthibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wala kisomo hakimfikii, kwa sababu Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَأَن لَّيْسَ لِلْإِنسَانِ إِلَّا مَا سَعَىٰ
“… mtu hatopata [malipo] isipokuwa yale aliyoyafanyia juhudi… ”[5]
Aayah ni yenye kuenea na haifanywi kuwa ni maalum isipokuwa kwa dalili maalum.
[1] al-Bukhaariy (2670) na Muslim (1004).
[2] Muslim (1631).
[3] Ahmad (2005) na Abu Daawuud (3310). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Abiy Daawuud” (2831). Hadiyth kama hiyo inapatikana katika al-Bukhaariy (1953) na Muslim (1148) tofauti muulizaji ni mwanaume.
[4] al-Bukhaariy (1952) na Muslim (1147).
[5] 53:39
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 216-217
- Imechapishwa: 03/08/2025
Swali: Mama yangu amefariki na nataka kumzawadia thawabu zangu. Je, nimuombee du´aa, nimsomee Qur-aan, nimtolee swadaqah au nimsomee al-Faatihah?
Jibu: Mtolee swadaqah. Bwana mmoja alimwambia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mama yangu amekufa. Nadhani kuwa lau angeliweza kutamka basi angetoa swadaqah. Je, nimtolee swadaqah?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Ndio.”[1]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Anapofariki mwanadamu basi matendo yake hukatika isipokuwa mambo matatu; swadaqah yenye kuendelea, elimu ambayo watu wananufaika nayo au mtoto mwema mwenye kumuombea du´aa.”[2]
Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) amepokea kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh kutoka kwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anh) ya kwamba kuna mwanamke alimuuliza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kama anatakiwa kulipa siku za mama yake za Ramadhaan? Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akajibu:
“Unaonaje lau mama yako angelikuwa na deni ungelimlipia nalo? Deni la Allaah lina haki zaidi kulipwa.”[3]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Anayekufa na ameacha swawm anayodaiwa, basi atafungiwa na walii wake.”[4]
Kuhusu kumsomea Qur-aan, kukiwemo al-Faatihah, ni jambo halikuthibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wala kisomo hakimfikii, kwa sababu Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَأَن لَّيْسَ لِلْإِنسَانِ إِلَّا مَا سَعَىٰ
“… mtu hatopata [malipo] isipokuwa yale aliyoyafanyia juhudi… ”[5]
Aayah ni yenye kuenea na haifanywi kuwa ni maalum isipokuwa kwa dalili maalum.
[1] al-Bukhaariy (2670) na Muslim (1004).
[2] Muslim (1631).
[3] Ahmad (2005) na Abu Daawuud (3310). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Abiy Daawuud” (2831). Hadiyth kama hiyo inapatikana katika al-Bukhaariy (1953) na Muslim (1148) tofauti muulizaji ni mwanaume.
[4] al-Bukhaariy (1952) na Muslim (1147).
[5] 53:39
Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 216-217
Imechapishwa: 03/08/2025
https://firqatunnajia.com/matendo-mema-kwa-ajili-ya-mamangu-aliyefariki/