Swali: Upande mmoja Allaah (´Azza wa Jall) anaeleza kuwa Ibraahiym (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
مَا هَـٰذِهِ التَّمَاثِيلُ الَّتِي أَنتُمْ لَهَا عَاكِفُونَ
”Nini haya masanamu ambayo nyinyi mnayakalia kuyaabudu?”[1]
Upande mwingine Allaah (´Azza wa Jall) amesema kuhusu maaskari wa Sulaymaan (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
يَعْمَلُونَ لَهُ مَا يَشَاءُ مِن مَّحَارِيبَ وَتَمَاثِيلَ وَجِفَانٍ كَالْجَوَابِ وَقُدُورٍ رَّاسِيَاتٍ ۚ اعْمَلُوا آلَ دَاوُودَ شُكْرًا ۚ وَقَلِيلٌ مِّنْ عِبَادِيَ الشَّكُورُ
”Wanamfanyia kazi atakayo kujenga ngome ndefu za fakhari na masanamu na madeste makubwa kama mahodhi na masufuria makubwa yaliyothibiti imara. Fanyeni kazi, enyi familia ya Daawuud, kwa kushukuru – na wachache miongoni mwa waja Wangu ni wenye kushukuru!”[2]
Ni vipi tutaoanisha masanamu yaliyoharamishwa katika Aayah ya kwanza na katika Aayah ya pili ambapo wamezingatiwa kuwa ni neema alopewa?
Jibu: Masanamu yaliyotajwa katika Aayah kuhusu Ibraahiym (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kulikusudiwa kwa sababu yalikuwa yakiabudiwa. Masanamu yaliyotajwa kuhusu Sulaymaan (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kulikusudiwa kwa sababu ya pambo. Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
لِكُلٍّ جَعَلْنَا مِنكُمْ شِرْعَةً وَمِنْهَاجًا
“Kwa kila Ummah katika nyinyi Tumeujaalia Shari’ah na mfumo wake.”[3]
Yalikuwa yenye kuruhusiwa kwa Sulaymaan ambapo Shari´ah yetu ikaja kuyakataza. Mosi ni kwa sababu ya kuigiliza uumbaji wa Allaah, pili ni kwa sababu yanaabudiwa.
[1] 21:52
[2] 34:13
[3] 05:48
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 349-350
- Imechapishwa: 07/07/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
Related
43. Mitume wote walikuwa waja na watumwa wa Allaah
Mtunzi wa kitabu amesema: “Muhammad ni mja Wake aliyeteuliwa.” Yeye ni mja wa Allaah (´Azza wa Jall). Hana chochote katika haki ya uungu wala haki ya uola. Hakika si venginevyo yeye ni mja na Mtume wa Allaah anayetekeleza amri Zake, kujiepusha na makatazo Yake na mwenye kufikisha ujumbe kutoka kwa…
In "Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah - al-Fawzaan"
150. Usidanganyike na matendo yako
Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema: 123 – Ee Allaah! Wewe unayelinda Uislamu na waislamu! Tuthibitishe juu ya Uislamu mpaka pale tutapokutana Nawe tukiwa nao! MAELEZO Haya ni miongoni mwa maneno mazuri ya mtunzi wa kitabu (Rahimahu Allaah). Baada ya yeye kutaja masuala haya makubwa na ya khatari, akamuomba Allaah…
In "Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah - al-Fawzaan"
04. Kuogopa shirki
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema: 1- Allaah (´Azza wa Jall) amesema: إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ”Hakika Allaah hasamehi kushirikishwa na anasamehe yaliyo chini ya hayo kwa amtakae.”(04:48) 2- Ibraahiym (´alayhis-Salaam) amesema: وَاجْنُبْنِي وَبَنِيَّ أَن نَّعْبُدَ الْأَصْنَامَ “Uniepushe mimi na wanangu…
In "Sharh Kitaab-it-Tawhiyd - Ibn Baaz"