Swali: Je, ni katika Sunnah kusoma Suurah ”al-Kahf” siku ya ijumaa? Je, paja ni uchi?

Jibu: Kusoma Suurah ”al-Kahf” siku ya ijumaa kumepokewa baadhi ya Hadiyth zenye udhaifu, lakini zinatiana nguvu zenyewe kwa zenyewe. ´Abdullaah bin ´Umar (Radhiya Allaahu ‘anhumaa) alikuwa akifanya hivo.

Kwa hiyo akiisoma Suurah ”al-Kahf” siku ya ijumaa ni jambo jema.

Kuhusu paja ni uchi kwa mujibu wa mtazamo wa wanzuoni wengi. Kwa hiyo anapaswa kulifunika ndani ya swalah na mbele ya watu pia.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (29/221)
  • Imechapishwa: 26/02/2026