Swali: Ni ipi hukumu ya josho la ijumaa?
Jibu: Josho la ijumaa wanachuoni wametofautiana. Kikosi cha wanachuoni wengi wanaona kuwa ni jambo limependekezwa. Hilo ni kutokana na Hadiyth isemayo:
“Ambaye atatawadha siku ya ijumaa ni vyema. Na ambaye ataoga ndio bora zaidi.”
Wanachuoni wengine wakaona kuwa ni jambo la lazima. Wamejengea hoja kwa Hadiyth ya Abu Sa´iyd isemayo:
“Josho la ijumaa ni wajibu kwa kila mwenye kuota.”
Hadiyth hii ni Swahiyh zaidi kuliko yenye kusema:
“Ambaye atatawadha siku ya ijumaa ni vyema… “
Wapo wanachuoni wengine wenye kuona kuwa kuoga ni lazima kwa wale wafanya kazi pasi na wengine. Wamejengea hoja kwa Hadiyth ya ´Aaishah isemayo:
“Watu walikuwa wanakuja siku ya ijumaa ambapo wanatokwa na harufu kwa sababu walikuwa ni wafanya kazi. Ndipo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akawaambia:
“Laiti mngelioga.”
Kwa hivyo masuala haya kuna maoni tatu tofauti ya wanachuoni. Jopo la wanachuoni wengi wanaona kuwa imependekezwa na mapendekezo yanakuwa na nguvu zaidi ikiwa mtu ataoga.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (18)
- Imechapishwa: 01/01/2021
Swali: Ni ipi hukumu ya josho la ijumaa?
Jibu: Josho la ijumaa wanachuoni wametofautiana. Kikosi cha wanachuoni wengi wanaona kuwa ni jambo limependekezwa. Hilo ni kutokana na Hadiyth isemayo:
“Ambaye atatawadha siku ya ijumaa ni vyema. Na ambaye ataoga ndio bora zaidi.”
Wanachuoni wengine wakaona kuwa ni jambo la lazima. Wamejengea hoja kwa Hadiyth ya Abu Sa´iyd isemayo:
“Josho la ijumaa ni wajibu kwa kila mwenye kuota.”
Hadiyth hii ni Swahiyh zaidi kuliko yenye kusema:
“Ambaye atatawadha siku ya ijumaa ni vyema… “
Wapo wanachuoni wengine wenye kuona kuwa kuoga ni lazima kwa wale wafanya kazi pasi na wengine. Wamejengea hoja kwa Hadiyth ya ´Aaishah isemayo:
“Watu walikuwa wanakuja siku ya ijumaa ambapo wanatokwa na harufu kwa sababu walikuwa ni wafanya kazi. Ndipo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akawaambia:
“Laiti mngelioga.”
Kwa hivyo masuala haya kuna maoni tatu tofauti ya wanachuoni. Jopo la wanachuoni wengi wanaona kuwa imependekezwa na mapendekezo yanakuwa na nguvu zaidi ikiwa mtu ataoga.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (18)
Imechapishwa: 01/01/2021
https://firqatunnajia.com/maoni-tatu-tofauti-juu-ya-josho-la-siku-ya-ijumaa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)