Mama wanaowatia vijimaneno na kuwaharibia ndoa wasichana wao

Swali: Je, huingia katika kumtia fitina mke mama wa mume au mama wa mke endapo atamuharibu msichana wake dhidi ya mume wake?

Jibu: Ni yenye kuenea; inamuhusu mume, inamuhusu mama yake, baba yake, kaka yake na jirani yakee. Ni yenye kumuhusu kila mtu.

Swali: Mama anaona kuwa jambo hilo ni kwa manufaa ya msichana wake na si kwa makusudi?

Jibu: Hapana; si halali hiajuzu kwake kumuharibu dhidi ya mume wake. Akikuwapo tatizo, waende kwa mume wamuombe amtaliki na wampatie pesa zake. Hapo ni pale wanapomuona mume hamstahiki.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/27667/هل-تدخل-ام-الزوجة-واهلها-في-وعيد-تخبيبها
  • Imechapishwa: 07/04/2025