Makabila ambayo mwanamke hamkalii eda mume wake

Swali: Kuna baadhi ya makabila katika Hijaaz kama vile Thaqiyf na kabila la Banuu Maalik, na kabila la Banuu al-Haarith, ambapo mwanamke kwao hamkalii eda mume wake wakati anapofariki. Ni ipi hukumu ya hilo?

Jibu: Hili kwa hali yoyote ni kutokana na ujinga. Ni lazima liondolewe kwa elimu, ni mamoja awe ni katika Banuu Maalik, Thaqiyf au wengineo. Walinganizi na mahakimu lazima wawafikishie watu na kuwaelekeza katika jambo hili wanalolijua vibaya, nalo ni kutokukaa eda; kwamba mwanamke hamkalii eda mume wake.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1252/هل-يجوز-للمراة-ترك-الاحداد-على-زوجها
  • Imechapishwa: 13/02/2026