Mahujaji au wenye kufanya ´Umrah walionuia kukaa zaidi ya siku nne Makkah

Swali: Ni ipi hukumu ya kufupisha swalah kwa anayefanya hajj wakati wa kukaa kwake Makkah zaidi ya siku nne?

Jibu: Ikiwa kukaa kwa mwenye kufanya hajj Makkah ni siku nne au chini ya hapo, basi Sunnah kwake ni kuswali swalah zenye Rak´ah nne kuziswali Rak´ah mbilimbili. Hivo ndivo alivyofanya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika hajj ya kuaga. Ama ikiwa amekusudia kukaa zaidi ya siku nne, basi lililo la tahadhari zaidi ni kuswali Rak´ah nne, maoni ambayo ndio ya kikosi kikubwa cha wanazuoni.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/201)
  • Imechapishwa: 12/03/2026