Swali: Ni vipi tutaoanisha kati ya maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Je, ni mfitini wewe, ee Mu´aadh?”
na kitendo chake yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa vile imethibiti ya kwamba alisoma al-Baqarah, Aal ´Imraan, al-Maaidah, al-A´raaf na nyenginezo?
Jibu: Makusudio yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kuhimiza kukhafifisha pindi mtu anapokuwa imamu anayewaswalisha watu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yeyote katika nyinyi atakayeswalisha watu basi akhafifishe. Hakika katika wao yupo mdogo, mtumzima, mnyonge na mwenye haja. Akiswali peke yake basi arefushe anavotaka.”[1]
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni mtu mwenye kukhafifisha swalah zaidi katika ukamilifu wake. Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Nimeswali nyuma ya mtu anayekamilisha swalah. Wala hakuna yeyote anayekhafifisha swalah kama Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[2]
Kuna maafikiano juu yake.
Lakini akiswali peke yake arefushe anavotaka.
Kisomo chake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) cha al-Baqarah, an-Nisaa´ na Aal ´Imraan ilikuwa ni katika swalah ya usiku.
[1] al-Bukhaariy (662) na Muslim (714).
[2] al-Bukhaariy (667) na Muslim (721).
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/90)
- Imechapishwa: 21/11/2021
Swali: Ni vipi tutaoanisha kati ya maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Je, ni mfitini wewe, ee Mu´aadh?”
na kitendo chake yeye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa vile imethibiti ya kwamba alisoma al-Baqarah, Aal ´Imraan, al-Maaidah, al-A´raaf na nyenginezo?
Jibu: Makusudio yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni kuhimiza kukhafifisha pindi mtu anapokuwa imamu anayewaswalisha watu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yeyote katika nyinyi atakayeswalisha watu basi akhafifishe. Hakika katika wao yupo mdogo, mtumzima, mnyonge na mwenye haja. Akiswali peke yake basi arefushe anavotaka.”[1]
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni mtu mwenye kukhafifisha swalah zaidi katika ukamilifu wake. Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Nimeswali nyuma ya mtu anayekamilisha swalah. Wala hakuna yeyote anayekhafifisha swalah kama Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[2]
Kuna maafikiano juu yake.
Lakini akiswali peke yake arefushe anavotaka.
Kisomo chake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) cha al-Baqarah, an-Nisaa´ na Aal ´Imraan ilikuwa ni katika swalah ya usiku.
[1] al-Bukhaariy (662) na Muslim (714).
[2] al-Bukhaariy (667) na Muslim (721).
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/90)
Imechapishwa: 21/11/2021
https://firqatunnajia.com/mahimizo-ya-kukhafifisha-swalah-na-wakati-huohuo-kuikamilisha/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)