Maelezo ya Hadiyth “Mwenye kupitwa na ´Aswr ni kama vile ameikosa familia na mali yake”

Swali 27: Nini maana ya Hadiyth:

“Mwenye kupitwa na ´Aswr ni kama vile ameikosa familia na mali yake.”?

Jibu: Mwenye kupitwa na ´Aswr kwa njia ya kwamba hakuiswali kwa wakati wake, ameshughulishwa nayo, amelala na mfano wake. Basi mtu huyo ni kama vile ameikosa familia na mali yake kwa msemo mwingine ni msiba mkubwa kutokuiswali ´Aswr kwa wakati wake. Haina maana kwamba mtu huyu anaacha kuswali kwa kukusudia.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ash-Sharh al-Mumtaaz, uk. 36
  • Imechapishwa: 01/11/2018