Swali: Vipi kuhusu madhambi ambayo mtu amekufa juu yake na hakutubia kwayo?
Jibu: Hukumu ni hiyohiyo kama ilivyokuja katika Hadiyth. Alipomsitiri duniani baina Yake na yeye atamsamehe (Subhaanahu wa Ta´ala). Pengine yakawa ni miongoni mwa yale madhambi madogo ambayo yanasamehewa kwa kujiepusha na madhambi madogo:
إِن تَجْتَنِبُوا كَبَائِرَ مَا تُنْهَوْنَ عَنْهُ نُكَفِّرْ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ
“Mkijiepusha madhambi makubwa mnayokatazwa Tutakufutieni madhambi yenu.”[1]
Mja anajiepusha na madhambi madogo na hivyo anasamehewa madhambi madogo. Huenda makosa hayo ameyafanya baina ya mja na Mola wake na hakuna ayajuaye isipokuwa tu Yeye (Subhaanahu wa Ta´ala) na mja hakuweza kutubia kwayo. Matokeo yake Allaah akamsamehe kwayo kutokana na mema na matendo yake mazuri ambayo ni mengi na Allaah kumridhia. Yale mema aliyoyafanya yanakuwa ni kama tone la maji baharini. Tone la uchafu kwenye bahari ya mambo ya kheri na hivyo Akamsamehe (Subhaanahu wa Ta´ala) kwayo.
[1] 04:31
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24472/حكم-ذنوب-المسلم-التي-مات-ولم-يتب-منها
- Imechapishwa: 23/10/2024
Swali: Vipi kuhusu madhambi ambayo mtu amekufa juu yake na hakutubia kwayo?
Jibu: Hukumu ni hiyohiyo kama ilivyokuja katika Hadiyth. Alipomsitiri duniani baina Yake na yeye atamsamehe (Subhaanahu wa Ta´ala). Pengine yakawa ni miongoni mwa yale madhambi madogo ambayo yanasamehewa kwa kujiepusha na madhambi madogo:
إِن تَجْتَنِبُوا كَبَائِرَ مَا تُنْهَوْنَ عَنْهُ نُكَفِّرْ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ
“Mkijiepusha madhambi makubwa mnayokatazwa Tutakufutieni madhambi yenu.”[1]
Mja anajiepusha na madhambi madogo na hivyo anasamehewa madhambi madogo. Huenda makosa hayo ameyafanya baina ya mja na Mola wake na hakuna ayajuaye isipokuwa tu Yeye (Subhaanahu wa Ta´ala) na mja hakuweza kutubia kwayo. Matokeo yake Allaah akamsamehe kwayo kutokana na mema na matendo yake mazuri ambayo ni mengi na Allaah kumridhia. Yale mema aliyoyafanya yanakuwa ni kama tone la maji baharini. Tone la uchafu kwenye bahari ya mambo ya kheri na hivyo Akamsamehe (Subhaanahu wa Ta´ala) kwayo.
[1] 04:31
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24472/حكم-ذنوب-المسلم-التي-مات-ولم-يتب-منها
Imechapishwa: 23/10/2024
https://firqatunnajia.com/madhambi-ambayo-muislamu-amekufa-kabla-ya-kutubia-kwayo/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
