Swali: Nini maana ya msemo:

”Hadiyth ngeni (حديث غريب)”?

Jibu: Hii maana yake kwa wanazuoni wakati mwingine huwa ni Hadiyth iliyokuja kwa njia moja tu. Wakati mwingine maana ya ngeni ni kwamba imekuja kwa njia ya fulani mwana wa fulani tu, ni ngeni kwa upande wake, lakini imepokewa na wengine pia. Kwa msemo mwingine si ngeni kwa ujumla. Huitwa ngeni kwa njia ya fulani, bi maana ni ugeni wa kuhusiana kwa wanazuoni wa Hadiyth.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1033/معنى-الحديث-الغريب
  • Imechapishwa: 08/01/2026