11 – Abu Ibraahiym Isma´iyl bin al-´Abbaas amesema:
“Nimemsikia Shaqiyq, mtumwa wa kiume wa al-Answaariy, akiulizwa kuhusu ndoto ya al-Answaariy juu ya ‘Amr bin ´Ubayd. Nikasema: “Ameota nini?” Amesimulia ya kwamba amesema: “Nimemuona akibadilika na kuwa tumbili na mnyororo shingoni mwa mchimba kaburi. Nikasema: “Ee Abu ´Uthmaan! Ni nini kimefanya kuwa hivi?” Akasema: “Maneno yangu juu ya makadirio.” Nikamuuliza al-Answaariy juu ya hilo na akasema: “Ee mwanangu mpendwa! Msitaje makosa ya wanazuoni.”
12 – ´Amr bin Swaalih al-Mukhtaar amesema:
“Nilikuwa kwa Hishaam bin Hassan wakati ´Amr bin ´Ubayd alipotajwa. Nikaona jinsi alivyokasirika. Akasema: Naapa kwa jina la Allaah kwamba hakuna kinachomzidishia mzushi isipokuwa ni kuwa mbali zaidi na Allaah kwa vitendo vyake na hakuna Allaah anachomzidishia isipokuwa kumkasirikia zaidi.”
13 – Ma´mar amesema:
“Ayyuub [as-Sikhtiyaaniy] alikuwa akisema: “Amefanya nini anayechukia ‘Amr bin ‘Ubayd? Sijawahi ‘Amr bin ‘Ubayd hata siku kuwa ni mwenye akili.”
14 – Sufyaan bin Mu´aadh bin Mu´aadh amesema:
“Nilizungumza na ´Amr bin ‘Ubayd juu ya mirathi ya mwanamke aliyetalikiwa kabisa. Nikawa najenga hoja dhidi yake kwa maoni ya ‘Uthman (Radhiya Allaahu ´anh) na kwamba anamruhusu yeye kurithi. Akasema: “Harithi kabisa.” Nikasema: “´Uthmaan ndio hoja yangu.” Akasema: “´Uthmaan hakuwahi kuwa hoja yoyote wala Sunnah.”
15 – ´Amr bin Nadhwr:
“Nilipita karibu na ‘Amr bin ‘Ubayd akiwa amekaa. Nikakaa naye. Akataja kitu na nikasema: “Hivyo hawasemi maswahiba zetu.” Akasema: “Maswahiba zako ni kina nani umkose baba yako?” Nikasema: ”Ayyuub, Yuunus, Ibn ´Awn na at-Taymiy.” Akasema: “Wao ni wachafu na najisi na wafu. Hawako hai.”
- Muhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy (afk. 385)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Akhbaar ´Amr bin ´Ubayd bin Baab al-Mu´taziliy, uk. 96-100
- Imechapishwa: 22/11/2025
11 – Abu Ibraahiym Isma´iyl bin al-´Abbaas amesema:
“Nimemsikia Shaqiyq, mtumwa wa kiume wa al-Answaariy, akiulizwa kuhusu ndoto ya al-Answaariy juu ya ‘Amr bin ´Ubayd. Nikasema: “Ameota nini?” Amesimulia ya kwamba amesema: “Nimemuona akibadilika na kuwa tumbili na mnyororo shingoni mwa mchimba kaburi. Nikasema: “Ee Abu ´Uthmaan! Ni nini kimefanya kuwa hivi?” Akasema: “Maneno yangu juu ya makadirio.” Nikamuuliza al-Answaariy juu ya hilo na akasema: “Ee mwanangu mpendwa! Msitaje makosa ya wanazuoni.”
12 – ´Amr bin Swaalih al-Mukhtaar amesema:
“Nilikuwa kwa Hishaam bin Hassan wakati ´Amr bin ´Ubayd alipotajwa. Nikaona jinsi alivyokasirika. Akasema: Naapa kwa jina la Allaah kwamba hakuna kinachomzidishia mzushi isipokuwa ni kuwa mbali zaidi na Allaah kwa vitendo vyake na hakuna Allaah anachomzidishia isipokuwa kumkasirikia zaidi.”
13 – Ma´mar amesema:
“Ayyuub [as-Sikhtiyaaniy] alikuwa akisema: “Amefanya nini anayechukia ‘Amr bin ‘Ubayd? Sijawahi ‘Amr bin ‘Ubayd hata siku kuwa ni mwenye akili.”
14 – Sufyaan bin Mu´aadh bin Mu´aadh amesema:
“Nilizungumza na ´Amr bin ‘Ubayd juu ya mirathi ya mwanamke aliyetalikiwa kabisa. Nikawa najenga hoja dhidi yake kwa maoni ya ‘Uthman (Radhiya Allaahu ´anh) na kwamba anamruhusu yeye kurithi. Akasema: “Harithi kabisa.” Nikasema: “´Uthmaan ndio hoja yangu.” Akasema: “´Uthmaan hakuwahi kuwa hoja yoyote wala Sunnah.”
15 – ´Amr bin Nadhwr:
“Nilipita karibu na ‘Amr bin ‘Ubayd akiwa amekaa. Nikakaa naye. Akataja kitu na nikasema: “Hivyo hawasemi maswahiba zetu.” Akasema: “Maswahiba zako ni kina nani umkose baba yako?” Nikasema: ”Ayyuub, Yuunus, Ibn ´Awn na at-Taymiy.” Akasema: “Wao ni wachafu na najisi na wafu. Hawako hai.”
Muhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy (afk. 385)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Akhbaar ´Amr bin ´Ubayd bin Baab al-Mu´taziliy, uk. 96-100
Imechapishwa: 22/11/2025
https://firqatunnajia.com/kwenye-kilele-cha-mutazilah-amr-bin-ubayd-iii/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
