Kwanini asikufurishwe anayepinga uchawi?

Swali: Wasemaje kwa mwenye kusema:

“Uchawi ni ukhurafi na ni jambo lisilokuwa na uhakika”?

Jibu: Mwenye kufanya hivi ni kafiri. Kwa kuwa Allaah Ametaja uchawi katika Qur-aan na akaubainisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Uchawi upo na ni hakika. Baadhi yake ni hakika, unamfanya mtu kuwa mgonjwa na kuua, na baadhi yake ni kiini macho (mazingaombwe). Wote ni ukafiri. Mwenye kuupinga anakuwa kafiri, kwa kuwa ameikadhibisha Qur-aan.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://subulsalam.com/play.php?catsmktba=14579
  • Imechapishwa: 21/11/2014