Swali: Kuwaswalia Mitume wakati wanapotajwa katika Aayah?

Jibu: Sijui ubaya wowote wa kufanya hivo. Hata hivyo bora ni kuacha kufanya hivo katika swalah ya faradhi. Lakini akifanya hivo basi jambo ni lenye wasaa. Kwa mujibu wa kanuni baadhi ya wanazuoni wanaona kuwa swalah ya faradhi ni kama swalah ya kujitolea. Kwa ajili hiyo Hanaabilah wanaona kuwa mtu anaweza kufanya hivo hata katika swalah ya faradhi.

Swali: Vipi kuhusu kumuomba kinga Allaah ya Moto na kumuomba Pepo?

Jibu: Bora ni kuacha kufanya hivo katika swalah ya faradhi.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25283/حكم-الدعاء-والصلاة-على-الانبياء-اثناء-تلاوة-الصلاة
  • Imechapishwa: 24/02/2025