Swali: Nimemsikia al-Kabsiy akipendekeza kuwasomea Qur-aan wafu na khaswa makaburini. Ni ipi hukumu ya hilo?

Jibu: Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:

وَأَن لَّيْسَ لِلْإِنسَانِ إِلَّا مَا سَعَىٰ

“… mtu hatopata [malipo] isipokuwa yale aliyoyafanyia juhudi… ”[1]

Qur-aan imeteremshwa ili iwe ponyo kwa ajili ya miili na mioyo. Hatukufikiwa na khabari yoyote kwamba wakati wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) walikuwa wakiwasomea wafu. Msichana wake alikufa, ´Uthmaan bin Madh´uun akafariki na wengine wengi pasi na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuamrisha kuwasomea chochote katika Qur-aan.

[1] 53:39

  • Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 174-175
  • Imechapishwa: 15/02/2025