Swali: Baadhi ya watu wanawaalika watu chakula na wanawalazimisha kumsomea maiti Suurah ”al-Ikhlaasw”?
Jibu: Haina msingi wowote. Haina msingi wowote. Hakuna suala la kutengeneza chakula wala kusoma. Ama wakitengenezewa chakula na majirani zao au majirani wakawaletea zawadi, hilo ni zuri. Kama alivyowaamrisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) familia yake wawapelekee chakula watu wa Ja´far alipofariki, kwa sababu limewapata lililowashughulisha. Majirani wa maiti wakileta chakula cha jioni au cha mchana kwa familia ya maiti, hilo ni zuri. Lakini familia ya maiti kuandalia watu chakula na kuwakaribisha kwa sababu ya msiba, hapana. Hilo ni miongoni mwa matendo ya kipindi kabla ya kuja Uislamu.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/28497/حكم-الدعوة-لطعام-مع-قراءة-الاخلاص-للميت
- Imechapishwa: 20/04/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)