Kuusia fulani asifike kwenye mazishi yangu

Swali: Je, inajuzu kwa Muislamu kuandika katika wasia wake fulani asimuoshe na asihudhurie jeneza lake kwa kuwa alimfanyia ubaya duniani?

Jibu: Hapana, haijuzu. Haijuzu kufanya hivi. Dunia imeisha. Ni juu yake kusamehe. Ama kuhusu kuusia fulani amswalie kutokana na fadhila zake, hakuna neno. Ausie fulani amuoshe na amswalie kutokana na fadhila zake na maarifa yake ya Ahkaam za kuosha, hakuna neno kufanya hivi.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (72) http://www.alfawzan.af.org.sa/node/14085
  • Imechapishwa: 16/11/2014