Swali: Je, mtu ambaye ametumbukia ndani ya uzinzi kisha akatubu na baadaye akajisalimisha katika mahakama yasiyohukumu kwa hukumu ya Uislamu?
Jibu: Namshauri atubu kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Wanazuoni wamekinzana kama anatakiwa kujisalimisha mwenyewe ili aadhibiwe au bora kwake ni yeye ajisitiri na dhambi yake. Kinachodhihiri ni kwamba bora ni yeye kujisitiri na dhambi yake. Kisa cha Maa´iz kinatambulika pale ambapo alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akakiri dhambi yake ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwambia:
“Umekunywa pombe? Pengine umembusu peke yake.” Maa´iz akasema hapana ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Umemjamii?” Akajibu: “Ndio.” Hapo ndipo akaadhibiwa.”
Vile ninavoona ni kuwa bora ni yeye kujisitiri kwa dhambi yake na asiende mahakamani.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 246
- Imechapishwa: 02/04/2025
Swali: Je, mtu ambaye ametumbukia ndani ya uzinzi kisha akatubu na baadaye akajisalimisha katika mahakama yasiyohukumu kwa hukumu ya Uislamu?
Jibu: Namshauri atubu kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Wanazuoni wamekinzana kama anatakiwa kujisalimisha mwenyewe ili aadhibiwe au bora kwake ni yeye ajisitiri na dhambi yake. Kinachodhihiri ni kwamba bora ni yeye kujisitiri na dhambi yake. Kisa cha Maa´iz kinatambulika pale ambapo alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akakiri dhambi yake ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwambia:
“Umekunywa pombe? Pengine umembusu peke yake.” Maa´iz akasema hapana ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Umemjamii?” Akajibu: “Ndio.” Hapo ndipo akaadhibiwa.”
Vile ninavoona ni kuwa bora ni yeye kujisitiri kwa dhambi yake na asiende mahakamani.
Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 246
Imechapishwa: 02/04/2025
https://firqatunnajia.com/kutubu-baada-ya-uzinzi/