Kutoka katika darsa za wanachuoni na kwenda Twitter

Swali: Nilikuwa nikihudhuria darsa za wanachuoni na kusoma vitabu vya Kiislamu. Halafu nikapewa mtihani wa Twitter na uchambuzi wa kisiasa. Ninajua fika ya kwamba hili ni katika njama za Shaytwaan, vipi nitaachana na hilo na kushinda matamanio yangu?

Jibu: Suluhu ni nyepesi, rudi katika matendo uliyokuwemo mwanzoni na uachane na Twitter. Muombe Allaah Akulinde na kila kilicho na madhara kwako. Mtake Allaah msaada na wala usikate tamaa.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (30) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ighastah%20%20-%2025-12-1435.mp3
  • Imechapishwa: 16/06/2015