Kutangaza kitu chenye thamani kilichopotea msikitini

Swali: Nikipotewa na kitu chenye thamani ndani ya msikiti, je, inafaa kwangu kukitangaza ndani ya msikiti kwa sababu nina uhakika kuwa kimenipotea ndani ya msikiti?

Jibu: Hapana, haijuzu kufanya hivo ndani ya msikiti. Toka nje ya msikiti na utangaze. Yafanyike nje ya msikiti, na si ndani ya msikiti.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (31)
  • Imechapishwa: 27/02/2022