Swali: Ikiwa kuna mtu aliyekufa akiwa na ufisadi mwingi. Je, inafaa kuwatahadharisha wenzake waliobaki kutokana na matendo yake?
Jibu: Hakuna tatizo ikiwa ufisadi wake ulikuwa dhahiri na maasi yake yalikuwa wazi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati kulipopitishwa jeneza na Maswahabah wakamweleza kwa shari, naye akasema:
”Imewajibika.”
Hakuwakataza kufanya hivyo. Hili linafasiriwa kwa maana kwamba maasi ya mtu huyo yalikuwa dhahiri. Mtu ambaye maasi yake ni ya wazi hakuna usengenyi. Hakuna juu yake usengenyi.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25245/هل-يجوز-تذكير-الناس-بفساد-من-مات
- Imechapishwa: 20/02/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)