Swali: Je, kuna dalili inayokataza kuswali nyuma ya aliyelala?
Jibu: Hapana, hapana vibaya kufanya hivo.
Swali: Anajigeuzageuza ilihali amelala?
Jibu: Haidhuru.
Swali: Hakuzingatiwi kuwa ni kupita mbele ya mswaliji?
Jibu: Hapana, hakuzingatiwi kuwa ni kupita mbele ya mswaliji.
Swali: Kutoka kwake [´Aaishah] mbele ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakuzingatiwi ni kupita?
Jibu: Kutoka kwake hakuzingatiwi ni kupita. Unaweza kutoka kwenye godoro, ukatoka kwa upande wa kichwa chake.
Swali: Anasema kuwa alitoka upande wa miguu yake?
Jibu: Ni mamoja upande wa miguu yake au kichwa chake. Yote ni mamoja. Hakuitwi kuwa ni kupita. Kupita ni kule ambako mtu anatoka upande huu anaenda upande ule.
Swali: Imetajwa katika baadhi ya Hadiyth kwamba ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) alikuwa juu ya kitanda. Je, si kitanda chote…
Jibu: Yeye yuko juu ya kitanda. Alikuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anaposujudu basi yeye [´Aaishah] anakunja miguu yake mpaka inagusana na miguu yake na yeye amelala.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23670/حكم-الصلاة-خلف-الناىم-وتقلبه-امام-المصلي
- Imechapishwa: 26/03/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)