Swali: Je, wakati wa kuchinja tunatakiwa kusema:

قُلْ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي وَمَحْيَايَ وَمَمَاتِي لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ

”Sema: “Hakika swalah yangu na kichinjwa changu na uhai wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Allaah pekee, Mola wa walimwengu.”[1]

Jibu: Wakati wa kuchinja kawaida mtu anasema:

باسم الله

“Kwa jina la Allaah.”

Kuhusu kusema:

قُلْ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي وَمَحْيَايَ وَمَمَاتِي لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ

”Sema: “Hakika swalah yangu na kichinjwa changu na uhai wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Allaah pekee, Mola wa walimwengu.”

hayo yanasemwa katika kuchinjwa siku ya ´Iyd. Kile kinachochinjwa na yule mwenye kuhiji anasema:

الله أكبر

“Allaah ni mkubwa.”

Vichinjwa vyenginevyo aseme:

باسم الله

“Kwa jina la Allaah.”

[1] 06:162

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (05) http://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191110#219240
  • Imechapishwa: 15/09/2019