Swali: Vipi kuhusu yale yaliyotangaa kwa Umm Sulaym kufanya kusilimu kwa Abu Twalhah ndio mahari yake?
Jibu: Hivi ndivo wanavoona baadhi ya wanazuoni kwamba mwanamke kufanya kusilimu kwa mwanaume au kumfunza Qur-aan ndio mahari yake na kwamba hapana vibaya kwa hilo. Hata hivyo Aayah ilishuka baada ya hapo. Aayah ya an-Nisaa´ ambayo ni ya al-Madiynah:
أَن تَبْتَغُوا بِأَمْوَالِكُم
”… mtafute [kuwaoa] kwa mali zenu… ”[1]
inafahamisha kuwa ni lazima kuwepo mali. Kuna uwezekano vilevile kisa cha Umm Sulaym ni kabla ya kushuka kwa Aayah. Ni lazima kufaradhisha pesa ingawa zitakuwa kidogo:
أَن تَبْتَغُوا بِأَمْوَالِكُم
”… mtafute [kuwaoa] kwa mali zenu… ”
[1] 04:24
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23840/حكم-جعل-اسلام-الرجل-او-تعليم-القران-مهرا
- Imechapishwa: 18/05/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)