Swali: Nikisikiliza Qur-aan nazingatiwa ni kana kwamba nimeisoma?
Jibu: Hapana. Unazingatiwa kuwa umesikiliza na hukusoma. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَإِذَا قُرِئَ الْقُرْآنُ فَاسْتَمِعُوا لَهُ وَأَنصِتُوا لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ
“Inaposomwa Qur-aan basi isikilizeni na nyamazeni kimya ili mpate kurehemewa.” (07:204)
Kusikiliza kunakuwa kwa masikio na kusoma kunakuwa kwa mdomo. Kusoma ni bora kuliko kusikiliza. Kwa sababu ukisoma kila herufi moja ni jema moja na jema moja linalipwa kumi mfano wake.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ma´aalim Manhaj Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 45
- Imechapishwa: 19/06/2021
Swali: Nikisikiliza Qur-aan nazingatiwa ni kana kwamba nimeisoma?
Jibu: Hapana. Unazingatiwa kuwa umesikiliza na hukusoma. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَإِذَا قُرِئَ الْقُرْآنُ فَاسْتَمِعُوا لَهُ وَأَنصِتُوا لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ
“Inaposomwa Qur-aan basi isikilizeni na nyamazeni kimya ili mpate kurehemewa.” (07:204)
Kusikiliza kunakuwa kwa masikio na kusoma kunakuwa kwa mdomo. Kusoma ni bora kuliko kusikiliza. Kwa sababu ukisoma kila herufi moja ni jema moja na jema moja linalipwa kumi mfano wake.
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ma´aalim Manhaj Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 45
Imechapishwa: 19/06/2021
https://firqatunnajia.com/kusikiliza-kama-si-kama-mwenye-kusoma/