41- al-Qaadhwiy Husayn bin Ismaa´iyl ametuhadithia: Abus-Swaa-ib Saalim bin Junaadah ametuhadithia: ´Abdullaah bin Numayr ametuhadithia, kutoka kwa ´Ubaydullaah bin ´Umar, kutoka kwa Sa´iyd bin Abiy Sa´iyd, kutoka kwa Abu Hurayrah aliyesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Lau nisingeliona uzito juu ya Ummah wangu basi ningeliwaamrisha kutumia Siwaak pamoja na wudhuu´ na ningechelewesha swalah ya ´Ishaa mpaka theluthi ya usiku au nusu ya usiku. Hakika Allaah (´Azza wa Jall) wakati huo hushuka katika mbingu ya dunia na kusema: “Je, kuna mwenye kuomba nimuitikie? Je, kuna mwenye kuomba nimpe maombi yake? Je, kuna mwenye kuomba msamaha nimsamehe?”
- Muhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Kitaab-un-Nuzuul, uk. 124
- Imechapishwa: 27/01/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket