24- Abu Bakr an-Naysaabuuriy ametuhadithia: Muhammad bin ´Abdil-Malik ametuhadithia: Ya´quub bin Ibraahiym bin Sa´d ametuhadithia: Baba yangu amenihadithia, kutoka kwa Abu Salamah bin ´Abdir-Rahmaan, kutoka kwa Abu ´Abdillaah al-Agharr, kutoka kwa Abu Hurayrah, kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyesema:

“Allaah (´Azza wa Jall) anashuka kila usiku katika mbingu ya dunia wakati kunapobaki theluthi ya mwisho ya usiku na anasema mpaka alfajiri inaingia: “Ni nani mwenye kuniomba nimuitikie? Ni nani aniombae maghfirah nimghufurie? Ni nani aniulizaye nimpe?”

  • Mhusika: Imaam ´Aliy bin ´Umar ad-Daaraqutwniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-un-Nuzuul, uk. 108
  • Imechapishwa: 01/01/2020