Kusalimiana kwa mikono na shangazi na mama zake wadogo wa mke

Swali: Je, inajuzu nimsalimie kwa kushikana mikono na shangazi na mama wadogo wa mke wangu?

Jibu: Haijuzu kwako kusalimiana kwa kushikana mikono, si kwa shangazi zake, mama wadogo zake wala hata dada zake. Huna ruhusa ya kufanya hivyo. Hili linaruhusiwa tu kwa mama wa mke na msichana wake baada ya ndoa kukamilika. Ama shangazi zake, mama wadogo zake na dada zake si Mahram kwako. Hivyo unasalimia kwa maneno tu:

“as-Salaam ´alaykum. Mna hali gani?” ambapo wanajibu, bila ya kushikana mikono.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/3185/حكم-مصافحة-عمات-وخالات-الزوجة
  • Imechapishwa: 30/07/2026