Kusafiri kwenda mazishini na kutoa pole

Swali: Ni ipi hukumu ya kusafiri kwa ajili ya kumswalia maiti au kwa ajili ya kutoa pole?

Jibu: Ni jambo halina msingi. Haikupokelewa kwamba Salaf walisafiri kwa ajili ya kutoa pole. Wewe lengo lako ni kumuombea yule maiti, unaweza ukamuombea popote ulipo. Khaswa hii leo unaweza kumpa pole kwa njia ya simu na wewe ukiwa mahala pako.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (15) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Umdah-24-11-1434_0.mp3
  • Imechapishwa: 15/09/2019