Swali: Ni ipi hukumu ya mtu kuomba sifa miongoni mwa sifa za Allaah?
Jibu: Haijuzu kuomba sifa. Mtu anatakiwa kufanya Tawassul kwazo:
”Ee Allaah! Ninakuomba kwa kukupenda kwangu, najilinda kwa radhi Yako kutokana na ghadhabu Zako na kwa msamaha Wako kutokana na adhabu Yako.”
Mtu anafanya Tawassul kwazo. Haifai kuziomba:
”Ee jicho la Allaah, tufanyie kadhaa! Ee mkono wa Allaah, turuzuku! Ee maneno ya Allaah, tusaidie!”
Haifai. Bali mtu aseme:
”Ee Allaah! Ee Mwingi wa rehema! Ee Mwenye kurehemu!”
Anaombwa kwa majina Yake (Jalla wa ´Alaa). Sifa haziombwi kwa maafikiano ya waislamu. Hivo ndivo alivyosema Shaykh-ul-Islaam (Rahimahu Allaah). Mtu anatakiwa kufanya Tawassul kwazo na kuomba ulinzi kwazo:
”Ee Allaah! Hakika mimi najilinda kwa radhi Yako kutokana na ghadhabu Zako na kwa msamaha Wako kutokana na adhabu Yako. Nakutaka msaada kwa rehema Yako, ee Mola wangu.”
Na mfano wa hayo.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/30980/هل-يجوز-دعاء-الصفة-من-صفات-الله
- Imechapishwa: 19/09/2025
Swali: Ni ipi hukumu ya mtu kuomba sifa miongoni mwa sifa za Allaah?
Jibu: Haijuzu kuomba sifa. Mtu anatakiwa kufanya Tawassul kwazo:
”Ee Allaah! Ninakuomba kwa kukupenda kwangu, najilinda kwa radhi Yako kutokana na ghadhabu Zako na kwa msamaha Wako kutokana na adhabu Yako.”
Mtu anafanya Tawassul kwazo. Haifai kuziomba:
”Ee jicho la Allaah, tufanyie kadhaa! Ee mkono wa Allaah, turuzuku! Ee maneno ya Allaah, tusaidie!”
Haifai. Bali mtu aseme:
”Ee Allaah! Ee Mwingi wa rehema! Ee Mwenye kurehemu!”
Anaombwa kwa majina Yake (Jalla wa ´Alaa). Sifa haziombwi kwa maafikiano ya waislamu. Hivo ndivo alivyosema Shaykh-ul-Islaam (Rahimahu Allaah). Mtu anatakiwa kufanya Tawassul kwazo na kuomba ulinzi kwazo:
”Ee Allaah! Hakika mimi najilinda kwa radhi Yako kutokana na ghadhabu Zako na kwa msamaha Wako kutokana na adhabu Yako. Nakutaka msaada kwa rehema Yako, ee Mola wangu.”
Na mfano wa hayo.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/30980/هل-يجوز-دعاء-الصفة-من-صفات-الله
Imechapishwa: 19/09/2025
https://firqatunnajia.com/kuomba-sifa-ya-allaah/