Swali: Ambaye anachelea juu ya nafsi yake na kuona kwamba asiponyoa ndevu zake atafungwa?
Jibu: Hapana. Hayo ni katika shaytwaan na shaytwaan kumtia khofu. Lakini akitenzwa nguvu jambo lake linajulikana hata kama inahusiana na shirki:
مَن كَفَرَ بِاللَّـهِ مِن بَعْدِ إِيمَانِهِ إِلَّا مَنْ أُكْرِهَ وَقَلْبُهُ مُطْمَئِنٌّ بِالْإِيمَانِ
“Atakayemkufuru Allaah baada ya kuamini kwake – isipokuwa yule aliyetenzwa nguvu na huku moyo wake umetua juu ya imani.”[1]
Kulazimishwa ambako mtu anapigwa kuna hukumu yake.
Muulizaji: Yeye anaogopa tu?
Ibn Baaz: Hapana, sio udhuru. Unafikri kuwa kutenzwa nguvu inakuwa namna hii tu?
Muulizaji: Kutenzwa nguvu inakuwa kwa kitendo?
Jibu: Inakuwa kwa kupigwa, kufungwa jela na kutishiwa kutoka kwa mtu aliye na uwezo.
[1] 16:106
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23891/حكم-حلق-اللحية-لمن-خاف-على-نفسه
- Imechapishwa: 25/05/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)