Swali: Kundi la wafanyakazi wanasikia adhaana kisha wanaswali mkusanyiko ndani ya kampuni. Je, kitendo chao hiki ni sahihi?
Jibu: Ni wajibu juu ya wanaume wote kuswali pamoja na mkusanyiko msikitini. Haijuzu kwao kuswali majumbani mwao wala mahali pa kazi ikiwa msikiti uko karibu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yeyote mwenye kusikia mwito kisha asiutikie, basi hana swalah isipokuwa kwa udhuru.” Akaulizwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa): ”Udhuru ni nini?” Akasema: “Khofu au maradhi.”
Bwana mmoja kipofu alimjia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akasema: ”Ee Mtume wa Allaah! Mimi sina wa kuniongoza kwenda msikitini. Je ninayo ruhusa niswali nyumbani kwangu?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Je unasikia mwito wa swalah?” Akasema: ”Ndio.” Akasema: “Basi itikia.”
Ameipokea Muslim katika ”as-Swahiyh” yake.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/120)
- Imechapishwa: 02/03/2026
Swali: Kundi la wafanyakazi wanasikia adhaana kisha wanaswali mkusanyiko ndani ya kampuni. Je, kitendo chao hiki ni sahihi?
Jibu: Ni wajibu juu ya wanaume wote kuswali pamoja na mkusanyiko msikitini. Haijuzu kwao kuswali majumbani mwao wala mahali pa kazi ikiwa msikiti uko karibu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yeyote mwenye kusikia mwito kisha asiutikie, basi hana swalah isipokuwa kwa udhuru.” Akaulizwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa): ”Udhuru ni nini?” Akasema: “Khofu au maradhi.”
Bwana mmoja kipofu alimjia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na akasema: ”Ee Mtume wa Allaah! Mimi sina wa kuniongoza kwenda msikitini. Je ninayo ruhusa niswali nyumbani kwangu?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Je unasikia mwito wa swalah?” Akasema: ”Ndio.” Akasema: “Basi itikia.”
Ameipokea Muslim katika ”as-Swahiyh” yake.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/120)
Imechapishwa: 02/03/2026
https://firqatunnajia.com/kundi-la-wafanyakazi-wanaswali-kazini/
Mshirikishe mwenzako:
- Share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Print (Opens in new window) Print
- Email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Share on X (Opens in new window) X
- Share on Pocket (Opens in new window) Pocket