Kumzungumzisha mtu baada ya kumaliza Adhkaar za kulala

Swali: Vipi mtu akimwongelesha mtu baada ya kumaliza kusoma Adhkaar za usiku?

Ibn Baaz: Amesimama kwa sababu ya haja?

Muulizaji: Kutokana na haja au akamuitikia mtu.

Jibu: Akisimama kwa sababu ya haja kisha akarudi, amemaliza na lengo limefikiwa. Akizirudia zote lengo limefikiwa. Hata hivyo lengo limefikiwa pale mwanzo tu atakapouweka ubavu wake chini. Ni sawa akazirudia wakati atakaposimama kutokana na haja au akamzungumzisha mtu. Vinginevyo lengo limekwishafikiwa.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23107/حكم-من-اتى-باذكار-النوم-ثم-قام-لحاجة
  • Imechapishwa: 03/11/2023