Swali: Mama yangu mimi sio msomi na hajui kusoma wala kuandika. Je, inafaa kwangu kusoma Qur-aan tukufu na kuswali swalah za sunnah na kumzawadia thawabu zake? Ni mambo gani ninayoweza kumzawadia thawabu zake ikiwa haijuzu?
Jibu: Hakuna dalili inayokubalika katika Shari´ah juu ya kumzawadia mwengine swalah na kisomo cha Qur-aan. Ni mamoja mtu huyo yuhai au ameshakufa. ´Ibaadah ni kwa kukomeka; hakuna kinachokubalika katika Shari´ah isipokuwa kile ambacho Shari´ah imefahamisha juu ya kusuniwa kwake. Lakini imesuniwa kwako kumwombea du´aa, kumtolea swadaqah, kumhijia na kumfanyia ´umrah akiwa ni mtumzima ambaye hawezi kuhiji wala kufanya ´umrah.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (09/321)
- Imechapishwa: 18/07/2021
Swali: Mama yangu mimi sio msomi na hajui kusoma wala kuandika. Je, inafaa kwangu kusoma Qur-aan tukufu na kuswali swalah za sunnah na kumzawadia thawabu zake? Ni mambo gani ninayoweza kumzawadia thawabu zake ikiwa haijuzu?
Jibu: Hakuna dalili inayokubalika katika Shari´ah juu ya kumzawadia mwengine swalah na kisomo cha Qur-aan. Ni mamoja mtu huyo yuhai au ameshakufa. ´Ibaadah ni kwa kukomeka; hakuna kinachokubalika katika Shari´ah isipokuwa kile ambacho Shari´ah imefahamisha juu ya kusuniwa kwake. Lakini imesuniwa kwako kumwombea du´aa, kumtolea swadaqah, kumhijia na kumfanyia ´umrah akiwa ni mtumzima ambaye hawezi kuhiji wala kufanya ´umrah.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (09/321)
Imechapishwa: 18/07/2021
https://firqatunnajia.com/kumzawadia-mzazi-asiye-msomi-thawabu-za-swalah-na-kisomo-cha-qur-aan/