Swali: Je, mtu amtakie radhi Abu Sufyaan (Radhiya Allaahu ´anhu) wakati yanapotajwa matendo yake yaliyowadhuru waislamu?
Jibu: Ndugu! Kulipitika kwa makafiri yaliyo mabaya zaidi kuliko matendo ya Abu Sufyaan na wakati waliposilimu wakawa wanatakiwa radhi. Kulipitika kwa ´Umar kabla ya kusilimu kwake na kadhalika. Uislamu unafuta yaliyo kabla yake.
قُل لِّلَّذِينَ كَفَرُوا إِن يَنتَهُوا يُغْفَرْ لَهُم مَّا قَدْ سَلَفَ
“Sema [uwaambie wale] waliokufuru: “Wakikoma basi watasamehewa yaliyopita.” (08:38)
Vipi unamtia aibu kwa kitu ambacho Allaah Amemsamehe kwacho? Haijuzu kufanya hivi kwa Abu Sufyaan wala mwengine asiyekuwa yeye.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (58) http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13521
- Imechapishwa: 16/11/2014
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)