Swali: Kabla ya mume kufa mke amemsamehe mume wake kwa sababu ya kuegemea kwake kwa mke mwingine. Je, atakuja siku ya Qiyaamah hali ya kuwa bega lake moja limepinda[1] au Allaah amekwishamsamehe?
Jibu: Sio kumili huko kulikokusudiwa. Hawezi kuwa mwadilifu inapokuja katika suala la mapenzi:
وَلَن تَسْتَطِيعُوا أَن تَعْدِلُوا بَيْنَ النِّسَاءِ وَلَوْ حَرَصْتُمْ
“Wala hamtoweza kufanya uadilifu kati ya wake japokuwa mtatupia.”[2]
Bi maana katika mapenzi. Ama kufanya uadilifu katika matumizi, mavazi, kugawa zamu usiku na makazi kunamlazimu. Kuna uadilifu unaowezekana, uadilifu usiowezekana.
[1] Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Ambaye yuko na wake wawili na akaegemea kwa mmoja wao, basi atakuja siku ya Qiyaamah hali ya kuwa bega lake moja limepinda.” (Abu Daawuud (2133), at-Tirmidhiy (1141) na Ibn Maajah (1969)).
[2] 4:129
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (41)
- Imechapishwa: 28/06/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)