Swali: Je, inajuzu kumkataza waziri miongoni mwa mawaziri juu ya minbari wakati anapofanya maovu miongoni mwa maovu au nasaha inakuwa siri kama inavokuwa kwa mtawala?

Jibu: Kuna faida gani kumkataza waziri juu ya minbari? Hakuleti faida yoyote. Kinacholeta ni fitina tu. Ukiona kosa kwa waziri miongoni mwa mawaziri mfikishie kwa kuwaendea na uwafikishie wasimamizi juu ya kosa hilo au mpe ujumbe kwa anayeweza kumfikishia.

Kuhusu kuzungumzia hilo juu ya minbari linaleta madhara zaidi kuliko inavoleta manufaa – ikiwa kama ndani yake kuna manufaa kweli.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: at-Tafsiyr al-Mufasswal (21) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tf–1428-2-22.mp3
  • Imechapishwa: 19/08/2020