Swali: Yule anayesema kwamba kumhama mtu ni kama dawa. Kama kunaleta manufaa, basi ndiko kutumike na kama…
Jibu: Ndio, ikiwa kunaleta manufaa, hutumika. Kama vile Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alivyowahama wale watu watatu na Allaah akawanufaisha kwa hilo. Lakini hakumhama ‘Abdullaah bin Ubayy na wenzake, kwa sababu kuhama hakukuwa na manufaa kwao.
Swali: Vipi mtu wa Bid´ah ikiwa mawaidha na uongofu havina athari kwake?
Jibu: Anahamwa.
Swali: Vipi ikiwa kumhama hakumletei manufaa?
Jibu: Ikiwa ipo dola inayosimamisha mambo kwa mujibu wa amri za Allaah, basi jambo lake linafikishwa kwa dola hiyo. Ama wewe binafsi, jukumu lako ni moja kati ya mawili: ama unampa nasaha au unamhama. Lakini huna ruhusa ya kumuua au kumpiga.
Swali: Katika hali hiyo kuhama kumewekwa katika Shari´ah?
Jibu: Ndio, hadi atakapotubia. Hata kama itachukua mwaka mmoja, miwili au hata miaka kumi, mpaka atakapotubia. Ni kama Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alivyowakata wale watu watatu kwa muda wa siku khamsini, mpaka Allaah alipokubali tawba yao.
Swali: Maana yake ni kwamba hakuna muda maalum wa kuhama?
Jibu: Ndio, khaswa inapokuja ikiwa ni katika maasi na Bid´ah.
Swali: Je, inategemea manufaa?
Jibu: Inategemea vile atakavyoona mwenye kuhama; akiona kwamba kutohama kutaleta manufaa kwao, basi aendelee kuonana nao na kuwapa nasaha. Lakini akiona kwamba nasaha hazina faida tena, basi anawahama.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31626/ما-ضابط-الهجر-النافع-للعاصي-والمبتدع
- Imechapishwa: 12/11/2025
Swali: Yule anayesema kwamba kumhama mtu ni kama dawa. Kama kunaleta manufaa, basi ndiko kutumike na kama…
Jibu: Ndio, ikiwa kunaleta manufaa, hutumika. Kama vile Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alivyowahama wale watu watatu na Allaah akawanufaisha kwa hilo. Lakini hakumhama ‘Abdullaah bin Ubayy na wenzake, kwa sababu kuhama hakukuwa na manufaa kwao.
Swali: Vipi mtu wa Bid´ah ikiwa mawaidha na uongofu havina athari kwake?
Jibu: Anahamwa.
Swali: Vipi ikiwa kumhama hakumletei manufaa?
Jibu: Ikiwa ipo dola inayosimamisha mambo kwa mujibu wa amri za Allaah, basi jambo lake linafikishwa kwa dola hiyo. Ama wewe binafsi, jukumu lako ni moja kati ya mawili: ama unampa nasaha au unamhama. Lakini huna ruhusa ya kumuua au kumpiga.
Swali: Katika hali hiyo kuhama kumewekwa katika Shari´ah?
Jibu: Ndio, hadi atakapotubia. Hata kama itachukua mwaka mmoja, miwili au hata miaka kumi, mpaka atakapotubia. Ni kama Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alivyowakata wale watu watatu kwa muda wa siku khamsini, mpaka Allaah alipokubali tawba yao.
Swali: Maana yake ni kwamba hakuna muda maalum wa kuhama?
Jibu: Ndio, khaswa inapokuja ikiwa ni katika maasi na Bid´ah.
Swali: Je, inategemea manufaa?
Jibu: Inategemea vile atakavyoona mwenye kuhama; akiona kwamba kutohama kutaleta manufaa kwao, basi aendelee kuonana nao na kuwapa nasaha. Lakini akiona kwamba nasaha hazina faida tena, basi anawahama.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31626/ما-ضابط-الهجر-النافع-للعاصي-والمبتدع
Imechapishwa: 12/11/2025
https://firqatunnajia.com/kumhama-mzushi-na-mtenda-maasi-ni-kama-dawa/