Swali: Ni ipi hukumu ya kumchukua picha maiti kwenye kanda ya video kisha mtu akauza kwa hoja kwamba anataka kuwakumbusha watu kifo?
Jibu: Ikiwa anakusudia kumchukua picha maiti wakati anapooshwa ni jambo ambalo halijuzu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza kuchukua picha viumbe vyenye roho na amemlaani mtengeneza picha pale aliposema:
“Ndio watu wataokuwa na adhabu kali siku ya Qiyaamah.”
Lakini ikiwa malengo ya muulizaji ni kutaka kubainisha namna anavyooshwa maiti kama Allaah alivyoweka katika Shari´ah katika kanda itakayotawanywa au kuuzwa hapana vibaya. Ni kama ambavo kunarekodiwa kuwafunza watu swalah na mengineyo miongoni mwa yale mambo ambayo watu wanayahitajia.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (08/425)
- Imechapishwa: 06/07/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)