Kulipa kafara kwa nguo nyepesi mno inayoonyesha ndani

Swali: Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema kuwa nguo inayojuzu kutoa katika kafara ni ile ambayo mtu anaweza kuswalia nayo. Tunaona kuwa kanzu zetu nyeupe hii leo zaonyesha ndani yake uchi ikiwa mtu hakuvaa nguo ya ndani…

Jibu: Hii haisihi. Hii ni nguo nyepesi mno inayoonyesha ndani. Haisihi, kwa sababu haisihi kuswali nayo. Haifuniki uchi na kwa ajili hiyo haitoshi kwa njia ya kuitolea kafara. Ile nguo ambayo haisihi kuswali nayo haisihi katika kuitolea kafara.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (42)
  • Imechapishwa: 28/06/2024