Kuleta Adhkaar baada ya swalah kwa pamoja kwa sauti ya juu

Swali: Je, inajuzu kwa imamu kusema Aayaat-ul-Kursiy kisha atasbiha mara tisini na tisa, kisha watu wakaitikia baada yake?

Jibu: Hapana. Kila mmoja peke yake. Kila mtu amtaje Allaah mwenyewe. Sio imamu kusema kisha wao wamfuate. Imamu peke yake na kila mmoja peke yake.

Swali: Vipi ikiwa ataona watu wanafanya hivyo?

Jibu: Awafundishe kwamba hilo halijahifadhiwa. Awalinganie kwa Allaah na awafundishe watu kheri. Awaambie kwamba hilo halijahifadhiwa, ee ndugu zangu, na kwamba kila mmoja amtaje Allaah kati yake na nafsi yake.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com’
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1390/حكم-ترديد-الاذكار-بعد-الصلاة-بصوت-جماعي
  • Imechapishwa: 13/12/2025