Kula kiwindwa kilichouliwa kwa gari, jiwe au fimbo

Swali: Ni ipi hukumu ya mtu aliyemuua sungura, paa au ndege kwa jiwe, fimbo au akamkanyaga kwa gari? Ni ipi hukumu ya kula mnyama huyo?

Jibu: Asimle. Akimkanyaga kwa gari, amempiga kwa jiwe au kwa fimbo, asimle. Huwa ni aliyeuawa kwa kupigwa, na si halali. Lakini ikiwa amemuua kwa bastola, akamwachia mbwa aliyefundishwa akamuua au akampiga kwa risasi, huku akisema:

بسم الله والله أكبر

”Kwa jina la Allaah. Allaah ni mkubwa.”

wakati wa kupiga, basi inaruhusiwa.

Swali: Vipi mwenye kuua kwa kurusha jiwe?

Jibu: Hapana vibaya ikiwa jiwe lina makali.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1370/حكم-اكل-صيد-قتل-بغير-محدد
  • Imechapishwa: 13/12/2025