Swali: Mwenye kusema kwamba hakufuru mtu mpaka akusudie kutoka nje ya Uislamu kwa maneno au matendo yake?
Jibu: Huyu ni mjinga. Afundishwe kwamba kufuru inaweza kuwa kwa moyo, mdomo au matendo. Wale waliosema:
“Hatujawaji kuona mfano wa wasomaji wetu hawa.”[1]
walikufuru kwa maneno.
Swali: Mwenye kusema hivi anakuwa Murji-ah?
Jibu: Murji-ah wanaona kinyume na hivi. Wanaona kuwa imani inakuwa kwa moyo na kwa mdomo. Lakini hawaoni kuwa haya hayaitwi ´imani`. Wanaona kuwa swalah na zakaah ni wajibu. Lakini haviitwi kuwa ni ´imani`. Hili ni kosa.
[1] at-Twabariy (10/172).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kashf-is-Shubuhaat, uk. 135
- Imechapishwa: 16/09/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)