Swali: Unasemaje juu ya yule mwenye kusema kwamba kufunga siku sita za Shawwaal ni Bid´ah na kwamba haya ni maoni ya Imaam Maalik? Akipewa dalili ya Hadiyth ya Abu Ayyuub:
“Atakayefunga Ramadhaan kisha akaifuatishia siku sita za Shawwaal basi ni kama ambaye amefunga mwaka mzima.”[1]
anasema kwamba katika cheni ya wapokezi wake kuna mtu ambaye ametiwa dosari.
Jibu: Maneno haya ni batili. Hadiyth ya Abu Ayyuub ni Swahiyh. Hadiyth hiyo ina zengine zenye kuisapoti na kutolea dalili maana yake.
[1] Muslim (1164), at-Tirmidhiy (759), Abu Daawuud (2433), Ibn Maajah (1716), Ahmad (05/417) na ad-Daarimiy (1754).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (15/390)
- Imechapishwa: 08/06/2018
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)