Kuendelea kazi ya haramu na huku mtu anatafuta nyingine

Swali: Mtu huyu anafanya kazi ya haramu na anahitajia pesa na wakati huohuo anatafuta kazi ya halali. Je, inajuzu kwake kuendelea kubaki katika kazi hii ya haramu mpaka pale atapopata kazi ya halali?

Jibu: Hapana. Hapana. Haijuzu kufanya kazi ya haramu. Chumo lake ni haramu. Haijuzu kufanya hivi. Ni juu yake kutafuta riziki na akimbilie kutafita riziki safi:

وَمَن يَتَّقِ اللَّـهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ

“Na yeyote yule anayemcha Allaah, basi atamjaalia njia ya kutokea na atamruzuku kutoka njia ambayo hatizamii.” (65:02-03)

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Duruus-ul-Haram http://www.alfawzan.af.org.sa/node/15208
  • Imechapishwa: 28/06/2020