Kuchelewesha kulisha chakula juu ya deni la Ramadhaan

Swali: Yule ambaye anawajibikiwa kulisha chakula masikini kwa ajili ya siku alizoacha kufunga katika Ramadhaan, je, anapaswa kulisha siku hiyohiyo ambayo hakufunga au hakuna tatizo kwake kuchelewesha mpaka baada ya Ramadhaan?

Jibu: Anaweza kuitanguliza na anaweza kuichelewesha. Anaweza kuifanya mwishoni mwa mwezi, na anaweza kuitoa katikati ya mwezi. Hii ni ikiwa ni mgonjwa ambaye hatarajiwi kupona au ni mzee wa makamo.

  • Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (24)
  • Imechapishwa: 18/09/2026