Swali: Nina mwenzangu kazini (karakana ya magari) ninamwita kwenda kuswali, lakini anakataa kwa hoja kwamba nguo zake si safi na ni vigumu kwake kuzibadilisha na kwamba ataswali atakaporudi makazi yake. Ni ipi hukumu ya kitendo chake hichi?
Jibu: Ni wajibu kwa huyo mwenzako aliyetajwa kuswali pamoja na mkusanyiko. Haijuzu kwake kuchelewesha swalah mpaka arudi nyumbani kwake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yeyote mwenye kusikia mwito kisha asiutikie, basi hana swalah isipokuwa kwa udhuru.” Akaulizwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa): ”Udhuru ni nini?” Akasema: “Khofu au maradhi.”
Udhuru ni maradhi na mfano wake. Ama kusema kwamba nguo ni chafu sio udhuru. Lakini kama ziko na najisi, basi ni wajibu kwake kuziosha au kuzibadilisha kwa nguo zilizo twahara. Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) awaongoze wote.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/121)
- Imechapishwa: 02/03/2026
Swali: Nina mwenzangu kazini (karakana ya magari) ninamwita kwenda kuswali, lakini anakataa kwa hoja kwamba nguo zake si safi na ni vigumu kwake kuzibadilisha na kwamba ataswali atakaporudi makazi yake. Ni ipi hukumu ya kitendo chake hichi?
Jibu: Ni wajibu kwa huyo mwenzako aliyetajwa kuswali pamoja na mkusanyiko. Haijuzu kwake kuchelewesha swalah mpaka arudi nyumbani kwake. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yeyote mwenye kusikia mwito kisha asiutikie, basi hana swalah isipokuwa kwa udhuru.” Akaulizwa Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa): ”Udhuru ni nini?” Akasema: “Khofu au maradhi.”
Udhuru ni maradhi na mfano wake. Ama kusema kwamba nguo ni chafu sio udhuru. Lakini kama ziko na najisi, basi ni wajibu kwake kuziosha au kuzibadilisha kwa nguo zilizo twahara. Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) awaongoze wote.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (30/121)
Imechapishwa: 02/03/2026
https://firqatunnajia.com/kuacha-kuswali-msikitini-kwa-hoja-ya-nguo-chafu/
Mshirikishe mwenzako:
- Share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Print (Opens in new window) Print
- Email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Share on X (Opens in new window) X
- Share on Pocket (Opens in new window) Pocket