Hadiyth hii kubwa ambapo Mu´aadh anabainisha yale Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyomtuma kwa watu wa Yemen kuna faida zifuatazo:
Kitu cha kwanza wanacholinganiwa watu ni kushuhudia ya kwamba hapana mungu wa haki ispokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah. Hili ndio jambo la kwanza kabla ya kila kitu. Unapowaendea makafiri kuwalingania usianze kwa kuwaambia waache pombe, uzinzi na ribaa. Hili ni kosa. Anza kwa msingi wa misingi kwanza kisha ndio uende kwenye tanzu. Kitu cha kwanza unachotakiwa kulingania ni katika Tawhiyd na ujumbe; washuhudie ya kwamba hapana mungu wa haki ispokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah. Halafu baada ya hapo mbainishie nguzo zingine za dini kisha ufuatishie lililo muhimu zaidi ya lingine na kuteremka.
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Riyaadh-is-Swaalihiyn (02/502-503)
- Imechapishwa: 10/09/2025
Hadiyth hii kubwa ambapo Mu´aadh anabainisha yale Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliyomtuma kwa watu wa Yemen kuna faida zifuatazo:
Kitu cha kwanza wanacholinganiwa watu ni kushuhudia ya kwamba hapana mungu wa haki ispokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah. Hili ndio jambo la kwanza kabla ya kila kitu. Unapowaendea makafiri kuwalingania usianze kwa kuwaambia waache pombe, uzinzi na ribaa. Hili ni kosa. Anza kwa msingi wa misingi kwanza kisha ndio uende kwenye tanzu. Kitu cha kwanza unachotakiwa kulingania ni katika Tawhiyd na ujumbe; washuhudie ya kwamba hapana mungu wa haki ispokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Mtume wa Allaah. Halafu baada ya hapo mbainishie nguzo zingine za dini kisha ufuatishie lililo muhimu zaidi ya lingine na kuteremka.
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Riyaadh-is-Swaalihiyn (02/502-503)
Imechapishwa: 10/09/2025
https://firqatunnajia.com/kitu-cha-kwanza-kafiri-analinganiwa-nacho-ni-tawhiyd/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
