Kisomo cha Qur-aan juu ya roho ya baba aliyefariki

Swali: Kuna mtu amefiwa na baba yake. Bwana mmoja akampa pesa 100 ili asome Qur-aan na thawabu zimwendee baba yake. Ni ipi hukumu ya chukua pesa hizi? Thawabu zinamfikia yule maiti?

Jibu: Hiyo ni Bid´ah. Haikuthibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pindi alipofariki msichana wake Zaynab, mtoto wake wa kiume kutoka kwa Maariyah, Hamzah, ´Uthmaan bin Madh´uun na jopo la Maswahabah wengine ya kwamba alipeana pesa ili watu wasome Qur-aan kwa kumkusudia fulani. Huo ni ujanja wa kuchukua pesa za watu kwa batili.

Kuhusu Hadiyth inayosema:

“Hakika ambacho kina haki zaidi ya kuchukuliwa malipo ni Kitabu cha Allaah.”

ni Swahiyh. Hata hivyo mtu afupizike kutokana na sababu yake kutokana na dalili nyenginezo ambazo ni katika matabano.

  • Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 326
  • Imechapishwa: 29/04/2025