Kifungamanishi ni lazima kitajwe na kiapo ili kifanye kazi

Swali: Vipi ikiwa mtu ataapa kisha baada ya dakika moja au mbili akaongezea neno “Allaah akitaka”?

Jibu: Ili kiapo kiwe kimetundikwa inahitajia kifungamanishi kitajwe pamoja na kiapo. Mapumziko kati ya kiapo na kifungamanishi haiathiri kitu ikiwa inahusiana na kukohoa au haja nyingine. Hata hivyo kifungamanishi hakifanyi kazi ikiwa mapumziko hayana sababu. Hainufaishi kitu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Fath-il-Majiyd (23) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/tahid-25-07-1435-01.mp3
  • Imechapishwa: 11/02/2017